Kadi za harusi za kidijitali Tanzania

Tuma kadi za harusi kwa kila mgeni kwa WhatsApp na SMS, ujue nani amethibitisha kuja, na uscan kadi zao pindi watakapofika ukumbini. Sisi tunafanya kila kitu, wewe furahia sherehe.

Kwanini watu hawatumi mialiko ya harusi tena, kwa kadi za karatasi?

Kadi za karatasi ni ghali, zinachelewa kufika, na zinapotea. Hapa kwetu karibu kila mtu yupo WhatsApp, kwa hiyo kadi ikitumwa kwenye simu inamfikia mgeni papo hapo na wewe unajua nani ameipata. Hakuna kuprint, hakuna kuhangaika ukijiuliza kama kadi ilimfikia mtu au la.

Kinachotutofautisha Mialiko ni kwamba hatukuachii kazi. Hutakaa kudesign kadi wala kutuma ujumbe mmoja mmoja. Wewe tupe taarifa, sisi tunadesign, tunatuma kwa kila mgeni, na siku ya harusi tunakusaidia ukumbini.

Tunavyofanya kazi

Kuanzia orodha ya wageni mpaka siku ya harusi, hatua tano tu.

Tupe taarifa na orodha ya wageni

Tuambie majina ya bwana na bibi harusi, tarehe, na ukumbi, kisha utupe orodha ya wageni. Huhitaji account wala app.

Tunadesign kadi yako

Timu yetu inadesign kadi ya harusi yako, na kila mgeni anapata kadi yenye jina lake na QR code yake.

Tunatuma kwa kila mgeni

Kila mgeni anapata kadi yake kwa WhatsApp. Asiye na WhatsApp anaipata kwa SMS, hakuna anayeachwa.

Unajua nani anakuja

Majibu yanaingia kwenye dashboard yako moja kwa moja. Unaona nani amekubali, nani amekataa, na nani bado hajajibu.

Unascan kadi wanapofika ukumbini

Siku ya harusi, unascan kadi ya kila mgeni anapofika ukumbini. Kwa harusi inayofanyika Tanzania, timu yetu inaweza kuja kukufanyia kazi hiyo.

Tools za bure za kupanga harusi

Anza kupanga leo, bila kujisajili.

Calculator ya bajeti ya harusi

Jua harusi yako itakugharimu kiasi gani kwa TZS.

Fungua calculator

Excel ya orodha ya wageni

Fomu tayari ya kuandika majina, namba za simu, na idadi ya watu.

Download fomu

Kadi za harusi za bure

Design za kadi tayari kwa harusi yako. Zinakuja hivi karibuni.

Angalia kadi

Maswali kuhusu kadi za harusi za kidijitali

Maswali ambayo watu hutuuliza kabla ya kuanza.

Hukupata unachotafuta? Wasiliana na timu yetu

Tuanze na harusi yako?

Tupe taarifa zako, mialiko yote tunashughulikia sisi.

Anza sasa